SIFA BIA ZA LUGHA

Lugha ni mfumo wa sauti na ishara za nasibu inayotumika jamii yenye utamaduni wao kwa mawasiliano.
Mfumo ina inadhihirisha kuwa lugha ina safu mbili kuu:
Maana
Sauti
Kila lugha ina fonolojia/sauti zake za pekee. Sauti mbalimbali hubainishwa na sifa mbalimbali.
Lugha ya binadamu pia hutumia ishara, kuna ishara za aina mbili:
Ishara za nasibu, ambazo hakuna uhusiano baina ya kitaja na kitajwa, mathalan; meza, kiti n.k
Ishara zisizo za nasibu, hapa kuna uhusiano baina ya kitaja na kitajwa, mathalan; tuktuk, Tingatinga n.k
Lugha hukitofautisha binadamu na Wanyama; sifa bia za lugha- inahusu sifa za lugha za binadamu ambayo hukitofautisha na Wanyama. Sifa hizo ni kama vile;
Umakinikaji, lugha humwezesha binadamu kuweza kuzungumza/ kujihusisha na mawasiliano hata ijapokuwa anajishughulisha na kazi zingine. Tofauti na Wanyama ni lazima wajishughulishe kikamilifu na shughuli zao, mathalan nyuki, ngombe n.k
Unasibu, inadhihirisha uhusiano baina ya kitaja na kitajwa, kiashiria na kiashiriwa. Kuna maneno mengi sana katika lugha ambayo hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kitaja na kitajwa kwa mfano, nyumba, mbwa, shule n,k hata hivyo kuna yale ambayo hudhihirisha uhusiano huo k.v tuktuk, pikipiki n.k
Kuongopa, lugha humwezesha binadamu kusema uongo, hata hivyo kuna kiwango kidogo ambapo Wanyama huonyesha uwezo huu kwa mfano; jogoo
Uzalishaji/ ubunaji, lugha ya binadamu humwezesha kuzalisha kauli nyingi zisizo kikomo kwa kuzingatia kanuni ya lugha husika.
Uhamishaji, lugha humwezesha binadamu kutoa kauli za wakati uliopita na pia kauli ambazo zitatimizwa baadaye.
Utamaduni, lugha hutumika na wanadamu wenye utamaduni mahususi, kila jamii hutumia lugha kulingana na kanuni walizoweka. Wanyama hawana utamduni.

0717558214- NICHOLAS ROP KIPLANG’AT



Leave a comment

About Me

Welcome to my blog, MTU KUZI, a space dedicated to informing and educating a diverse audience without bias toward age, gender, race, or any other distinguishing factor. I am a seasoned professional with a deep foundation in communication, translation, administration, and education. My extensive experience spans prestigious roles at institutions like Pwani University, Mozilla Foundation, KIPPRA, and teaching Kiswahili at the University of Carolina – Chapel Hill.As a Kiswahili expert, I specialize in translating between English and Kiswahili and tutor both languages with a focus on immersive, practical learning experiences. My expertise in Kiswahili not only enhances my teaching but also enriches my translations, allowing for culturally and contextually accurate communication.In this blog, I leverage my skills and experiences to create content that bridges cultural divides and fosters understanding. Proficient in various software applications and online collaboration platforms, I aim to streamline communication processes and engage with a global audience effectively.You are invited to join me on this journey of exploration and learning. Follow MTU KUZI on Facebook, Twitter, Instagram, and LinkedIn to stay updated and connected. Thank you for visiting, and I look forward to sharing more with you.

Newsletter